Adhabu Kali Katika Historia: Safari ya Maendeleo ya Haki za Binadamu.
Photo by Maria Pop on Pexels
Ulimwengu wa sasa umejawa na haki nyingi zaidi za binadamu ikilinganishwa na zamani ambapo mwenye nguvu ndiye aliyeko juu ya sheria na angeweza kumiliki hata roho yako wewe mnyonge na kuamua kuitoa atakapo na kwa njia aipendayo.
Katika Ulimwengu wa kale imeshuhudiwa mauaji ya kikatili zaidi kwa namna ya kutisha na kuleta hofu kwa watazamaji. Hii ilifanyika ili kufanya watawaliwa na raia wawe watiifu kwa viongozi wao pale wanapopewa maagizo ya kazi. Njia zilizotumika ni za mateso makubwa ya kinyama kwa binadamu.
Hapa tunakuletea njia tano katili zaidi za mauaji katika ulimwengu wa kale.
1. Kukalishwa juu ya ncha ya nguzo ya chuma iliyopakwa mafuta.
Njia hii imewahi kutumika Misri kuwaadhibu wahalifu ambapo nguzo hiyo ya chuma chenye ncha kali hupakwa mafuta na kuteleza kisha mhalifu akiwa amevuliwa nguo na kufungwa mikono na miguu hubebwa kisha kukalishwa juu ya nguzo hiyo. Kupitia njia ya haja kubwa nguzo hiyo hupenya kwa kuteleza hadi kutokea begani pembeni mwa shingo kwa sababu ya uzito wa mtu huyo.
2. Kuchunwa ngozi ukiwa hai.
Mbinu hii imewahi kutumika Ulaya na wakristo wa zamani kumuua mwanafalsafa mwanamke aliyefahamika kama Hypatia. Njia hii kama inavyojieleza inahusisha kumfunga mtu husika mikono na miguu kwa kamba kwenye nguzo mbele ya ukuta ili asiweze kusogea kisha kwa kutumia kisu kikali wanaanza kumchuna ngozi taratibu na mara nyingine kutumia maji moto kulainisha ngozi ili ichunike kirahisi. Kwa sababu ya upotevu wa damu na maumivu makali mtu huyo anazimia na hufariki baada ya masaa machache.
3. Kunyweshwa dhahabu ya moto iliyoyeyushwa. (uji wa dhahabu)
Mauaji haya yalitumika sana wakati wa dola la Warumi. Hapa mhalifu alifungwa mikono na miguu na kupanuliwa mdomo kwa kutumia vyuma maalumu kisha dhahabu ya moto iliyoyeyushwa (uji) humiminwa kupitia mdomoni kwenda tumboni. Uji huo wa dhahabu huharibu mfumo wote kuanzia mdomo, mapafu hadi tumboni na kuua papo kwa hapo.
4. Kuliwa na panya ukiwa hai.
Njia hii imewahi kutumika Uholanzi na Amerika ya kusini kuwatesa wafungwa.
Hapa mfungwa alilazwa juu ya ubao na mikono yake pamoja na miguu kufungwa, kisha panya waliofungiwa kweye wavu wa chuma hutengenezewa njia ya kutokea.
Wavu ule huwekwa juu ya tumbo la mfungwa huku ule mlango wa kutokea panya ukiwa umeelekezwa tumboni kwa mfungwa huyo na kushikizwa vizuri kwa waya ili usitikisike. Juu ya wavu makaa ya moto yaliwekwa na kuwafanya panya kusikia kuungua hivyo kutafuta njia rahisi ya kutokea, wakati huo njia ya kutokea imeelekezwa tumboni kwa mfungwa. Panya hulazimika kutafuta sehemu laini ya kutoboa ili wakimbie ambapo ni tumboni kwa mtu huyo, hivyo kutafuna ngozi ya tumbo hadi kuitoboa na kuingia ndani ya tumbo la mfungwa huyo. Panya hawa huleta maumivu makali na mateso ya hali ya juu pia hupelekea upotevu wa damu na kumuua mtu taratibu.
5. Kusimamishwa kwenye ndoo yenye zege.
Hii ilitumika Amerika ya kusini na Ugiriki ambapo muhalifu akiwa amefungwa mikono na miguu kwenye nguzo, miguu huingizwa kwenye ndoo iliyojaa zege kisha kuachwa hadi ligande. Njia pekee ya kujiokoa hapa ni kukata miguu. Hivyo mhalifu hushindwa kusogea na akizidiwa hutupwa majini na kufa.
Adhabu hizi za zamani zinatufundisha kuwa haki za binadamu tulizonazo leo si jambo la kawaida, bali ni matokeo ya mapambano ya muda mrefu dhidi ya ukatili na uonevu. Historia hutufundisha thamani ya utu, haki, na huruma. Ni jukumu letu kama kizazi cha sasa kuhakikisha kuwa hatuwezi kurudi nyuma, bali tuendelee kulinda hadhi ya kila mwanadamu.
Comments
Post a Comment